Wana TAWJA Tabora katika siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia. 

TAWJA Tabora kwa kushirikiana na dawati la jinsia, polisi leo tarehe 25/11/2025 wametoa elimu juu ya ukatili wa kijinsia mtandaoni, katika kituo cha Redio Uyui FM-Tabora.
Hii ni katika kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia. Katika picha ni Mhe Monika Muhandikila & Mhe Paulina Mkaumbya.

Mwenyekiti huyo ameeleza kwamba, katika Mkutano huo, Mahakama ya Tanzania itapata nafasi ya kutoa mada ya kuelezea hatua zinazochukuliwa na TAWJA katika kumpa nafasi mwanamke kwenye Uongozi hasa kwenye Mahakama.

Kaulimbiu ya Mkutano huo inasema ‘Nafasi ya Majaji Wanawake katika kupambana na mila potofu katika ulimwengu wa sasa.’

Mbali na TAWJA, Vyama vingine vitakavyoshiriki katika mkutano huo ni kutoka Nigeria, Kenya, Uganda, Afrika Kusini, Cote d’Ivoire na nyingine.

Kiongozi wa msafara wa wanachama wa TAWJA, Mhe. Sehel pamoja na wenzake wamewasili leo hii jijini Accra majira ya saa 5 asubuhi tayari kwa kushiriki kikamilifu Mkutano huo muhimu.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved