Author: admin

International Women’s Day

International Women’s Day

Today, as we celebrate the International Day of Women Judges, I am pleased to share an article that showcases the remarkable journeys of some inspiring women judges from Canada, El Salvador, the Republic of Korea, and a Deputy Registrar from the United Republic of Tanzania. These women share their paths in the judiciary and provide you with useful insights and advice. Their stories are a testament to the power of diversity and the important role women play in the judiciary around the world. At World Intellectual Property Organization – WIPO, we are committed to fostering an inclusive intellectual property (IP) and innovation ecosystem that supports innovation and creativity for the benefit of everyone, everywhere. Our WIPO Judicial Institute collaborates closely with judiciaries worldwide, providing tailored support that respects local traditions and enhances IP adjudication skills. These trailblazing women are not only advancing IP law within their regions but also inspiring future generations to join in building inclusive and dynamic IP systems.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved

MAJAJI, MAHAKIMU WANAWAKE WATOA ELIMU SIKU YA KIMATAIFA YA MAJAJI, MAHAKIMU MBEYA

MAJAJI, MAHAKIMU WANAWAKE WATOA ELIMU SIKU YA KIMATAIFA YA MAJAJI, MAHAKIMU MBEYA

Katika kusheherekea Siku ya Kimataifa ya Majaji na Mahakimu wanawake walitumia siku hiyo ya jana tarehe 10 Machi, 2025 kutoa elimu katika shule mbalimbali za Msingi na Sekondari za jiji la Mbeya.

Aidha, Shule zilizotembelewa katika zoezi hilo la utoaji elimu ni pamoja na Sangu High School, Samora Michel High School zilizopo katika Wilaya ya Mbeya na kutoa elimu kwa wanafunzi takribani 100,000 kutoka kwa waheshimiwa Majaji na Mahakimu Wanawake.

Waheshimiwa hao walitoa mada zilizoandaliwa na Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) zenye lengo la kuelimisha umma juu ya haki za msingi katika zama za kidigitali, huku wakifafanua mchango wa Majaji na Mahakimu Wanawake katika kushughulikia makosa ya unyanyasaji wa kimtandao kwa jinsia zote.

Waheshimiwa waliyoshiriki kutoa elimu hiyo walikuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Atuganile Ngwala, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya Mhe Zawadi Laizer, Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Mwanjelwa Mhe. Angela Kannyaninyi Byera, Mhe. Joyce Massawe, Hakimu mkazi mahakama ya Mwanzo Mwanjelwa, Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Iyunga Mhe. Hafsa Shelimo na Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Mbeya Mjini Mhe. Miriam Kamwaga.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved

Uzinduzi wa wiki ya sheria

TAWJA GALA DINNER 2025

TAWJA DODOMA, MOROGORO WAMPONGEZA JAJI LATIFA MANSOOR

TAWJA DODOMA, MOROGORO WAMPONGEZA JAJI LATIFA MANSOOR

Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) Dodoma na Morogoro wamepongeza Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Mhe. Latifa Alhinai Mansoor baada ya kuapishwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hafla ya uapisho iliyofanyika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 22 Januari, 2025.

Mhe Jaji Mansoor aliteuliwa tarehe 10 Januari, 2025 na Mhe. Rais Samia kuwa Jaji wa Mahakama hiyo. Kabla ya uteuzi huo, Jaji Mansoor alikuwa Jaji Mfawidhi, Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC), Morogoro.

Akizungumza na wanachama wa TAWJA kwa Mkoa wa Dodoma na Morogoro Mhe. Jaji Mansoor   amewashukuru wanachama hao kwa upendo na ushirikiano wao waliouonesha kwake.

“Namshukuru Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema kwa neema yake ya kunifanya nimetambuliwa na kunifanya niwe hivi nilivyo leo, sijui tamaduni za kule lakini ninaahidi nitafanya kazi kwa bidii kubwa ninamuomba Mwenyezi Mungu anipe afya ya kutosha ili niweze kutimiza majukumu yangu ipasavyo hasa kusimamia ukuaji, uboreshaji na utendaji kazi wa Mahakimu,” amesema Mhe. Jaji Mansoor.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo fupi Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo amempongeza Mhe. Mansoor na kumtakia kila lakheri katika majukumu yake, na kumuomba apokee zawadi ambayo ameandaliwa na wanachama wa TAWJA wa Mkoa wa Dodoma.

Akizungumza kwa niaba ya TAWJA Morogoro pamoja na watumishi wa Morogoro Naibu Msajili wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC), Morogoro Mhe. Susan Kihawa amempongeza Mhe. Jaji Mansoor kwa kuteuliwa kushika nafasi hiyo na kuahidi wataendeleza yale mazuri ambayo amewaachia.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na baadhi ya watumishi kutoka Dodoma na Morogoro.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved

MBIO MIAKA 25 YA TAWJA ZAFANA ARUSHA

MBIO MIAKA 25 YA TAWJA ZAFANA ARUSHA

Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) leo tarehe 19 Januari, 2025 kimefanya mbio maalum zilizohusisha Majaji, Naibu Wasajili, Mahakimu, vikundi vya riadha pamoja na Wadau mbalimbali ili kupinga vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 25 tangu kuanzishwa kwake.

Mbio hizo ambazo zilijumuisha umbali wa kilomita tano, 10 na 21 zilianza majira ya saa 12:30 Asubuhi kwenye viwanja vya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) na kuongozwa na Mgeni Rasmi, Mhe. Shally Joseph Raymond, Mbunge na Mwenyekiti wa Wabunge wanawake Bunge la Tanzania na pia Mwenyekiti wa Bunge la Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) ambaye amemwakilisha Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson pamoja na  Mlezi wa TAWJA, Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma.

Akitoa salaam mara baada ya kumalizika kwa mbio hizo, Mwakilishi huyo wa Mgeni Rasmi, Mhe. Shally Joseph Raymond amesema mila gandamizi kama ndoa za utotoni, ukeketaji wa wanawake (FGM), umiliki wa ardhi, nafasi za uongozi na maamuzi bado ni vikwazo katika kufikia usawa wa kijinsia na kwamba mila na tamaduni potofu ni changamoto kubwa inayosababisha kufisha ndoto za wengi katika kujiletea maendeleo ya kweli.

“Juhudi za pamoja na mbinu mbalimbali za kujikwamua kutoka katika madhila haya zinafanyika ili kubomoa mifumo gandamizi na kuvunja minyororo iliyojikita katika jamii zetu kwa karne nyingi. Hivyo, jubilei ya TAWJA ni tukio linalostahili kusherehekewa, siyo tu kwa sababu ya umri bali dira na dhima ya Chama tangu awali, ya kuwa mshumaa  wa mwanga na matumaini, ikipigania haki za kijinsia, hususani za wanawake na watoto,” amesema Mhe. Shally. 

Ametoa rai kwa TAWJA kuwa, inapoadhimisha miaka 25 pamoja na kujivunia mafanikio ni vema pia kutafakari kwa pamoja changamoto zinazoikabili jamii kwa kuwa bado kuna mila, tamaduni na mifumo gandamizi na nyingi zikiwa zimepitwa na wakati na vilevile wanawake na watoto bado wapo nyuma katika kulinda na kuteteta haki zao za msingi.

“Ni heshima kubwa sana kwangu kusimama mbele yenu leo, kama Mgeni Rasmi, katika tukio hili adhimu lililoandaliwa na Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA). Leo, hatushiriki tu katika mbio hizi bali ni sehemu ya harakati zinazolenga kuleta mabadiliko, kuzindua uelewa na kupinga masuala ya ukatili wa kijinsia (GBV) yaliyoshamiri na kukithiri katika jamii yetu,” ameeleza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA), Mhe. Barke Sehel amesema mbio hizo ni ishara ya kuanza kwa maadhimisho ya Jubilei ya miaka 25 ya TAWJA, pamoja na kuwashirikisha, kuhamasisha na kujenga uelewa kwa jamii na umma kuhusu hatua za kuchukua dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia (GBV) dhidi ya wanawake na Watoto.

“Ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa jamii ya Tanzania ina haki na inazingatia usawa kwa wote. Hivyo, tukio la leo, linathibitisha kwamba hatuko peke yetu katika kusimamia haki na usawa. Ni faraja kwangu kuona kuwa kwa pamoja tumeweza na tunaweza kuleta mabadiliko na kuhakikisha kuwa kila mwanamke na mtoto nchini Tanzania anapata haki na fursa anayostahili,” amesema Mhe. Sehel.

Mwenyekiti huyo amebainisha kuwa, TAWJA imekuwa ikijikita kwenye kukuza haki za binadamu na usawa kwa wote, hususan kwa wanawake, watoto na makundi maalum na kwamba wanapoadhimisha Jubilei ya miaka 25, TAWJA inajivunia kwa hatua kubwa ilifokia kwani imeweza kuletea mchango chanya kwenye jamii kwa upande wa haki.

Mhe. Sehel ameongeza kuwa, Chama hicho kimechangia kwenye mabadiliko ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, na kueleza kuwa, “TAWJA ilichukua juhudi za makususdi za kutoa elimu kwa wadau wa haki jinai, wabunge na jamii, kuhusu rushwa ya ngono (sextortion) na hivyo kuleta uelewa mpana katika jamii juu ya uwepo na athari ya vitendo vya rushwa ya ngono na hatimaye kubadilishwa kwa sheria kwa kuongeza kifungu maalum kuhusiana na rushwa ya ngono.”

Amesema baada yam bio hizo, wamepanga kutembela Shule za Sekondari sita, ambazo ni Ilboru, Arusha, Kimandolu, Kaloleni, Muriet na Sinoni kwa ajili ya kuanzisha Klabu za Haki za Kijinsia Mashuleni (Gender Justice Clubs) ambapo Wanachama wa TAWJA watapata fursa ya kutoa elimu kwa wanafunzi kuhusu kutambua aina zote za ukatili wa kijinsia, jinsi na wapi ya kuripoti ukatili wa kijinsia na kuwapa ujuzi muhimu wa maisha ikiwemo kuweka malengo ya kibinafsi na kujali afya na usafi wao.  

Mwenyekiti huyo ametoa shukran kwa Mahakama ya Tanzania, Mahkama ya Zanzibar, Kamati ya Maandalizi, wanachama wa TAWJA, wadau ambao ni UN Women, UNDP, WCF, PSSSF, Benki ya Equity, Jeshi la Polisi na Magereza, Hospitali ya Moyo, Vyama vya Riadha na wananchi wote waliojumuika kuungana nao na kufanikisha tukio hilo muhimu.

Mbio hizo zimebeba kaulimbiu, “Mshikamano katika Haki za Kijinsia Huanzia Hapa: “Shiriki na Elimisha.” Sambamba na hilo katika maadhimisho ya miaka 25 ya TAWJA kuna mabanda ya wadau mbalimbali likiwemo la Chama hicho ambao wanatoa elimu kuhusiana na huduma zao.

Ufunguzi wa Maadhimisho ya miaka 25 ya TAWJA unatarajiwa kufanyika kesho tarehe 20 Januari, 2025 ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved

MAJAJI, MAHAKIMU WANAWAKE TANZANIA KUSHIRIKI MKUTANO WA ‘IAWJ’ ACCRA GHANA

MAJAJI, MAHAKIMU WANAWAKE TANZANIA KUSHIRIKI MKUTANO WA ‘IAWJ’ ACCRA GHANA

Majaji na Mahakimu Wanawake wa Mahakama ya Tanzania wanatarajia kuungana na Majaji wanawake wenzao kutoka Ukanda wa Afrika kushiriki katika Mkutano wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Duniani (IAWJ) utakaofanyika jijini Accra nchini Ghana.

Akizungumza katika mahojiano maalum leo tarehe 12 Mei, 2024, Mwenyekiti wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) ambaye pia ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Barke Sehel amesema kuwa, Mkutano huo unatarajiwa kuanza rasmi kesho tarehe 13 hadi 18, Mei, 2024 na utafunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Ghana, Mhe. Nana Addo Dankwa Akufo-Addo.

“Mkutano huu ni wa Kikanda kwa Chama cha Majaji na Mahakimu wanawake, Mkutano huu unakutanisha wanachama Majaji na Mahakimu wanawake Afrika kwa ujumla. Kwa upande wa Tanzania tutakaoshiriki katika Mkutano huo ni 18 na idadi hii imejumuisha na wenzetu wa Zanzibar,” amesema Mhe. Sehel.

Mwenyekiti huyo ameeleza kwamba, katika Mkutano huo, Mahakama ya Tanzania itapata nafasi ya kutoa mada ya kuelezea hatua zinazochukuliwa na TAWJA katika kumpa nafasi mwanamke kwenye Uongozi hasa kwenye Mahakama.

Kaulimbiu ya Mkutano huo inasema ‘Nafasi ya Majaji Wanawake katika kupambana na mila potofu katika ulimwengu wa sasa.’

Mbali na TAWJA, Vyama vingine vitakavyoshiriki katika mkutano huo ni kutoka Nigeria, Kenya, Uganda, Afrika Kusini, Cote d’Ivoire na nyingine.

Kiongozi wa msafara wa wanachama wa TAWJA, Mhe. Sehel pamoja na wenzake wamewasili leo hii jijini Accra majira ya saa 5 asubuhi tayari kwa kushiriki kikamilifu Mkutano huo muhimu.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved

TAWJA celebrated International Day for Women Judges on 10th March, 2024 at Johari Rotana hotel

Access to Justices for Women and Children: Development and launch of Gender Bench Book

The Millennium Development Goal 3 Project: (MDG 3 Project) 

The Millennium Development Goal 3 Project: (MDG 3 Project) 

The MDG3 Project is generously funded by the Royal Government of the Netherland for Tanzania, Bosnia Herzegovina and the Philippines.

The Millennium Development Goals (MDGs) were developed out of the eight chapters of the United Nations Millennium Declarations signed in September, 2000.

The 8 goals are:-

  1. Eradicate extreme poverty and hunger
  2. Achieve universal primary education.
  3. Promote gender equality and empower women.
  4. Reduce child mortality.
  5. TeaImprove maternal health./li>
  6. Combat HIV/AIDS, malaria, and other diseases.
  7. Ensure environmental sustainability.
  8. Develop a global partnership for development.

The International Association of Women Judges is the implementing organization of the MDG3 Project in the three aforementioned countries, including Tanzania.

The IAWJ has coined a name for the Project. It is called Stopping Sexual Exploitation by Authority (Sextortion).

In March this year, TAWJA conducted MDG3 Sextortion Seminars for judges and magistrates in Arusha, Mtwara and Sumbawanga to disseminate human rights knowledge and skills particularly those relating to sexual abuse and exploitation by authority. The goal was to sensitize judicial officers to protect and promote human rights especially human dignity and respect in public institutions. 83 judges, magistrates and law enforcers participated in these seminars.

In May this year, TAWJA will conduct 3 MDG3 Sextortion seminars at the Institute of Judicial Administration in Lushoto, Tanga for 120 Second Year Diploma in Law students most of who are primary court magistrate trainees.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved