Author: admin
Ufunguzi wa Mafunzo ya waratibu wa TAWJA kutoka kila mkoa.
Ufunguzi wa Mafunzo ya waratibu wa TAWJA kutoka kila mkoa.
Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju amesema Majaji na Mahakimu Wanawake nchini wana wajibu mkubwa wa kusimamia haki za binadamu, maadili ya jamii na usawa wa kijinsia ili kuleta ustawi katika jamii.
Akizungumza jana tarehe 23 Oktoba, 2025 wakati akifungua Mafunzo kwa Waratibu wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) kwenye ukumbi wa Mikutnao wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma, Mhe. Masaju alisema kupitia mafunzo hayo ni muhimu wakaweka mikakati thabiti itakayowezesha kufikia ustawi katika jamii.
“Ninachoona ni kwamba ninyi TAWJA mnajitambua, wajibu wenu leo ni kuja na mikakati ambayo itawezesha kutatua hizi changamoto ambazo zimekuwa zinajitokeza kwenye haya masuala yanayowahusu na hasa haki za binadamu wote ambao humo wanajumuishwa Wanawake na Wanaume wakiwa wa umri mbalimbali, wengine watu wazima, wengine wazee na wengine Watoto kwa mfano kuna changamoto hii ya makosa unyanyasaji wa kijinsia,” alisema Jaji Mkuu.
Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) jana tarehe 23 Oktoba 2025 kimeanza kufanya mafunzo maalum kwa Waratibu wa Kikanda wa chama hicho, ambayo yamelenga kuimarisha uongozi, usimamizi na uwajibikaji katika kulinda haki za kijinsia na za binadamu.
Mafunzo hayo yalifanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma, ambapo mgeni rasmi alikuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa TAWJA ambaye pia ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Barke Sehel, alisema kuwa kufanyika kwa mafunzo hayo kuongeza uwezo wa Waratibu wa Mkoa katika uratibu, mawasiliano, na utekelezaji wa programu za kikanda.
“Tunatarajia kuwa kupitia waratibu hawa, TAWJA itaimarika na kuwa kinara katika ulinzi wa haki za binadamu na usawa wa kijinsia nchini,” alisema Mhe. Sehel.
TANZANIA WOMEN JUDGES ASSOCIATION.
Menu
© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved
Mhe George Mcheche Masaju, Jaji Mkuu wa Tanzania akizungumza na viongozi wa TAWJA
Mhe George Mcheche Masaju, Jaji Mkuu wa Tanzania akizungumza na viongozi wa TAWJA
TANZANIA WOMEN JUDGES ASSOCIATION.
Menu
© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved
MAKAO MAKUU YA TAWJA RASMI DODOMA
MAKAO MAKUU YA TAWJA RASMI DODOMA
Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA), Mhe. Barke Sehel amesema kuwa ofisi ya Makao Makuu ya chama hicho kwa sasa imehamia rasmi mkoani Dodoma.
Akiongoza kikao hivi karibuni cha wanachama wa TAWJA wa mkoani humo kilichofanyika katika ukumbi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Dodoma, Mhe. Sehel alisema kuwa, hatua ya kuhamia Dodoma kutarahisisha mawasiliano, kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa urahisi lakini pia kukuza utendaji wa kisekta ndani ya mfumo wa haki nchini.
“Namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma kwa neema yake ya kutufanya leo tumekutana hapa Dodoma na kuzungumza na wenzangu lakini pia nitumie fursa hii kuwajulisha kuwa kuanzia sasa ofisi ya TAWJA rasmi imehamia Dodoma na itakuwa katika Jengo la Makao Makuu ya Mahakama,” alisema Mhe. Sehel.
Akizungumza wakati wa kikao hicho, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma ambaye pia ni Mlezi wa Chama hicho kwa Kanda hiyo, Mhe. Dkt. Juliana Masabo aliwapongeza wanachama wote na kuwakaribisha wanachama wengine katika Mkoa wa Dodoma na kuahidi kushirikiana nao kwa kila kitu.
Nao Wajumbe wa TAWJA Kanda ya Dodoma, walipongeza juhudi za viongozi wa chama hicho kwamba, hatua hiyo italeta fursa mpya katika kushirikiana, kuongeza ufanisi na maendeleo katika mfumo wa utoaji haki pamoja na shughuli nyingine za kijamii.
Kikao hicho kilihudhuriwa na viongozi kutoka Mahakama ya Rufani ambao ni Majaji wakiongozwa na Mwenyekiti wa TAWJA Taifa, Mhe. Barke Sehel, Mhe Patricia Fikirini, Mhe. Lucy Kairo, Mhe. Zainab Muruke, Mhe Leila Mgonya pamoja na viongozi wengine wanawake kutoka Mahakama.
TANZANIA WOMEN JUDGES ASSOCIATION.
Menu
© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved
MKUTANO WA 17 WA IAWJ WAHITIMISHWA
MKUTANO WA 17 WA IAWJ WAHITIMISHWA
Mkutano wa 17 wa Chama cha Majaji Wanawake Duniani (IAWJ) umehitimishwa huku wanachama wa Chama hicho wakisisitizwa kufanya kazi kwa weledi na uadilifu.
Akifunga mkutano huo mwishoni mwa wiki iliyopita, Mwakilishi wa Jaji Mkuu wa Afrika Kusini ambaye ni Jaji wa Mahakama Kikatiba ya Nchi hiyo, Mhe. Nonkosi Mhlantla aliwataka washiriki wa mkutano huo kujithamini na kujipenda sambamba na kutosahau waliyojifunza wakati wote wa mkutano huo.
“Nawasihi kutosahau kupitia mliyojifunza mtapata uzoefu mzuri, Majaji mbalimbali walipata nafasi ya kuchangia uzoefu wao juu ya namna wanavyoshughulikia mashauri yanayohusu vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na mauaji ya wanawake, hivyo ni muhimu kujifunza na kuyaishi yote mazuri tuliyoyapata,” alisema Mhe. Mhlantla.
Jaji huyo aliwakumbusha Majaji na Mahakimu wanawake kujipenda na kujithamini kwanza ambapo alisema, “ni muhimu kujipenda na kujithamini, kufanya hivyo sio ubinafsi bali ni muhimu kufanya hivyo ili tuwe katika nafasi nzuri ya kutekeleza vizuri majukumu yetu ipasavyo,” alisisitiza.
Aidha, Jaji Mhlantla alisema kuwa, bado Mahakama nyingi hazina mbinu za kiusalama katika kuwalinda wahanga wa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia huku na kusema kwamba kuna haja ya kuchukua hatua thabiti ili kuwalinda watu hao.
Mgeni Rasmi huyo alizikumbusha pia nchi wanachama wa IAWJ kufanya uanaharakati ndani ya Mahakama hususani unaohusiana na matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) hususani akili unde ili kushughulikia matatizo mbalimbali yaliyopo ndani ya Mahakama ambayo ni pamoja na mlundikano wa mashauri.
Wakati wa mkutano huo uliofanyika kwa siku nne mada mbalimbali ziliwasilishwa ambazo ni pamoja na Majaji wanawake wanaongoza kuleta mabadiliko katika Mahakama za Kimataifa, Wanawake katika Uongozi-Mahali pa Kazi Usalama kwa Maafisa wa Mahakama, Ubaguzi na biashara haramu ya binadamu na nyingine.
Mada nyingine iliwasilishwa na Mhe. Edith Mwalukasa, Hakimu kutoka Mahakama ya Mwanzo Bagamoyo Tanzania mada hiyo ilijikita kuzungumzia ‘Athari za teknolojia katika masuala ya ukatili wa kijinsia.’
Aidha, wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa Chama hicho, wanachama wa IAWJ walifanya uchaguzi na kumchagua Rais mpya wa Chama hicho ambaye ni Mhe. Maria Filomena D. Singh kutoka nchini Morocco.
Mkutano huo ambao hufanyika kila baada ya miaka miwili umeazimia kuwa, Mkutano ujao wa mwaka 2027 utafanyikia nchini Canada.
TANZANIA WOMEN JUDGES ASSOCIATION.
Menu
© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved
TAWJA YAWASILI CAPE TOWN KUSHIRIKI MKUTANO MKUU WA MAJAJI WANAWAKE DUNIANI
TAWJA YAWASILI CAPE TOWN KUSHIRIKI MKUTANO MKUU WA MAJAJI WANAWAKE DUNIANI
Mkutano wa aina hii huwakutanisha pamoja Majaji na Mahakimu Wanawake Duniani kote na hufanyika kila baada ya miaka miwili na huwapa fursa Majaji hao kujadili masuala mbalimbali yanayohusu haki za wanawake, ukatili wa kijinsia, watoto na jamii kwa ujumla.
TANZANIA WOMEN JUDGES ASSOCIATION.
Menu
© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved
International Women’s Day
International Women’s Day
Today, as we celebrate the International Day of Women Judges, I am pleased to share an article that showcases the remarkable journeys of some inspiring women judges from Canada, El Salvador, the Republic of Korea, and a Deputy Registrar from the United Republic of Tanzania. These women share their paths in the judiciary and provide you with useful insights and advice. Their stories are a testament to the power of diversity and the important role women play in the judiciary around the world. At World Intellectual Property Organization – WIPO, we are committed to fostering an inclusive intellectual property (IP) and innovation ecosystem that supports innovation and creativity for the benefit of everyone, everywhere. Our WIPO Judicial Institute collaborates closely with judiciaries worldwide, providing tailored support that respects local traditions and enhances IP adjudication skills. These trailblazing women are not only advancing IP law within their regions but also inspiring future generations to join in building inclusive and dynamic IP systems.
TANZANIA WOMEN JUDGES ASSOCIATION.
Menu
© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved
MAJAJI, MAHAKIMU WANAWAKE WATOA ELIMU SIKU YA KIMATAIFA YA MAJAJI, MAHAKIMU MBEYA
MAJAJI, MAHAKIMU WANAWAKE WATOA ELIMU SIKU YA KIMATAIFA YA MAJAJI, MAHAKIMU MBEYA
Katika kusheherekea Siku ya Kimataifa ya Majaji na Mahakimu wanawake walitumia siku hiyo ya jana tarehe 10 Machi, 2025 kutoa elimu katika shule mbalimbali za Msingi na Sekondari za jiji la Mbeya.
Aidha, Shule zilizotembelewa katika zoezi hilo la utoaji elimu ni pamoja na Sangu High School, Samora Michel High School zilizopo katika Wilaya ya Mbeya na kutoa elimu kwa wanafunzi takribani 100,000 kutoka kwa waheshimiwa Majaji na Mahakimu Wanawake.
Waheshimiwa hao walitoa mada zilizoandaliwa na Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) zenye lengo la kuelimisha umma juu ya haki za msingi katika zama za kidigitali, huku wakifafanua mchango wa Majaji na Mahakimu Wanawake katika kushughulikia makosa ya unyanyasaji wa kimtandao kwa jinsia zote.
Waheshimiwa waliyoshiriki kutoa elimu hiyo walikuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Atuganile Ngwala, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya Mhe Zawadi Laizer, Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Mwanjelwa Mhe. Angela Kannyaninyi Byera, Mhe. Joyce Massawe, Hakimu mkazi mahakama ya Mwanzo Mwanjelwa, Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Iyunga Mhe. Hafsa Shelimo na Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Mbeya Mjini Mhe. Miriam Kamwaga.
TANZANIA WOMEN JUDGES ASSOCIATION.
Menu
© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved
Uzinduzi wa wiki ya sheria
Uzinduzi wa wiki ya sheria
TANZANIA WOMEN JUDGES ASSOCIATION.
Menu
© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved
TAWJA GALA DINNER 2025
TAWJA GALA DINNER 2025
TANZANIA WOMEN JUDGES ASSOCIATION.
Menu
© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved

















