Author: admin

MAKAO MAKUU YA TAWJA RASMI DODOMA

MAKAO MAKUU YA TAWJA RASMI DODOMA

Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA), Mhe. Barke Sehel amesema kuwa ofisi ya Makao Makuu ya chama hicho kwa sasa imehamia rasmi mkoani Dodoma.

Akiongoza kikao hivi karibuni cha wanachama wa TAWJA wa mkoani humo kilichofanyika katika ukumbi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Dodoma, Mhe. Sehel alisema kuwa, hatua ya kuhamia Dodoma kutarahisisha mawasiliano, kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa urahisi lakini pia kukuza utendaji wa kisekta ndani ya mfumo wa haki nchini.

“Namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma kwa neema yake ya kutufanya leo tumekutana hapa Dodoma na kuzungumza na wenzangu lakini pia nitumie fursa hii kuwajulisha kuwa kuanzia sasa ofisi ya TAWJA rasmi imehamia Dodoma na itakuwa katika Jengo la Makao Makuu ya Mahakama,” alisema Mhe. Sehel.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma ambaye pia ni Mlezi wa Chama hicho kwa Kanda hiyo, Mhe. Dkt. Juliana Masabo aliwapongeza wanachama wote na kuwakaribisha wanachama wengine katika Mkoa wa Dodoma na kuahidi kushirikiana nao kwa kila kitu.

Nao Wajumbe wa TAWJA Kanda ya Dodoma, walipongeza juhudi za viongozi wa chama hicho kwamba, hatua hiyo italeta fursa mpya katika kushirikiana, kuongeza ufanisi na maendeleo katika mfumo wa utoaji haki pamoja na shughuli nyingine za kijamii.

Kikao hicho kilihudhuriwa na viongozi kutoka Mahakama ya Rufani ambao ni Majaji wakiongozwa na Mwenyekiti wa TAWJA Taifa, Mhe. Barke Sehel, Mhe Patricia Fikirini, Mhe. Lucy Kairo, Mhe. Zainab Muruke, Mhe Leila Mgonya pamoja na viongozi wengine wanawake kutoka Mahakama.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved

MKUTANO WA 17 WA IAWJ WAHITIMISHWA

MKUTANO WA 17 WA IAWJ WAHITIMISHWA

Mkutano wa 17 wa Chama cha Majaji Wanawake Duniani (IAWJ) umehitimishwa huku wanachama wa Chama hicho wakisisitizwa kufanya kazi kwa weledi na uadilifu.

Akifunga mkutano huo mwishoni mwa wiki iliyopita, Mwakilishi wa Jaji Mkuu wa Afrika Kusini ambaye ni Jaji wa Mahakama Kikatiba ya Nchi hiyo, Mhe. Nonkosi Mhlantla aliwataka washiriki wa mkutano huo kujithamini na kujipenda sambamba na kutosahau waliyojifunza wakati wote wa mkutano huo.

“Nawasihi kutosahau kupitia mliyojifunza mtapata uzoefu mzuri, Majaji mbalimbali walipata nafasi ya kuchangia uzoefu wao juu ya namna wanavyoshughulikia mashauri yanayohusu vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na mauaji ya wanawake, hivyo ni muhimu kujifunza na kuyaishi yote mazuri tuliyoyapata,” alisema Mhe. Mhlantla.

Jaji huyo aliwakumbusha Majaji na Mahakimu wanawake kujipenda na kujithamini kwanza ambapo alisema, “ni muhimu kujipenda na kujithamini, kufanya hivyo sio ubinafsi bali ni muhimu kufanya hivyo ili tuwe katika nafasi nzuri ya kutekeleza vizuri majukumu yetu ipasavyo,” alisisitiza.

Aidha, Jaji Mhlantla  alisema kuwa, bado Mahakama nyingi hazina mbinu za kiusalama katika kuwalinda wahanga wa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia huku na kusema kwamba kuna haja ya kuchukua hatua thabiti ili kuwalinda watu hao.

Mgeni Rasmi huyo alizikumbusha pia nchi wanachama wa IAWJ kufanya uanaharakati ndani ya Mahakama hususani unaohusiana na matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) hususani akili unde ili kushughulikia matatizo mbalimbali yaliyopo ndani ya Mahakama ambayo ni pamoja na mlundikano wa mashauri.

Wakati wa mkutano huo uliofanyika kwa siku nne mada mbalimbali ziliwasilishwa ambazo ni pamoja na Majaji wanawake wanaongoza kuleta mabadiliko katika Mahakama za Kimataifa, Wanawake katika Uongozi-Mahali pa Kazi Usalama kwa Maafisa wa Mahakama, Ubaguzi na biashara haramu ya binadamu na nyingine.

Mada nyingine iliwasilishwa na Mhe. Edith Mwalukasa, Hakimu kutoka Mahakama ya Mwanzo Bagamoyo Tanzania mada hiyo ilijikita kuzungumzia ‘Athari za teknolojia katika masuala ya ukatili wa kijinsia.’ 

Aidha, wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa Chama hicho, wanachama wa IAWJ walifanya uchaguzi na kumchagua Rais mpya wa Chama hicho ambaye ni Mhe. Maria Filomena D. Singh kutoka nchini Morocco.

Mkutano huo ambao hufanyika kila baada ya miaka miwili umeazimia kuwa, Mkutano ujao wa mwaka 2027 utafanyikia nchini Canada.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved

TAWJA YAWASILI CAPE TOWN KUSHIRIKI MKUTANO MKUU WA MAJAJI WANAWAKE DUNIANI

TAWJA YAWASILI CAPE TOWN KUSHIRIKI MKUTANO MKUU WA MAJAJI WANAWAKE DUNIANI

Jumla ya Majaji na Mahakimu Wanawake 43 ambao ni wanachama wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) wamewasili katika Mji wa Cape Town nchini Afrika Kusini leo tarehe 08 Aprili, 2025 kushiriki katika Mkutano Mkuu wa 17 wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Duniani (IAWJ) unaotarajiwa kuanza kesho tarehe 09 Aprili, 2025.
Akizungumza katika mahojiano maalum leo tarehe 08 Aprili, 2025 mjini humo, Mwenyekiti wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA), Mhe. Barke Sehel amesema kuwa, Mkutano huo unatarajiwa kuanza rasmi kesho tarehe 09 hadi 12 Aprili, 2025 na Mgeni Rasmi katika mkutano huo anatarajiwa kuwa, Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Mhe. Matamela Cyril Ramaphosa.
“Mkutano huu ni wa Chama cha Majaji na Mahakimu wanawake Duniani, kwa ujumla unawakutanisha wanachama Majaji na Mahakimu wanawake duniani. Kwa upande wa Tanzania tutakaoshiriki katika Mkutano huo ni wanachama 43 idadi hii imejumuisha na wenzetu wa Zanzibar,” amesema Mhe. Sehel.
Kaulimbiu ya Mkutano huo inasema; ‘Wanawake na uongozi katika kushughulikia unyanyasaji wa kijinsia na mauaji ya dhidi ya wanawake.’
Mhe. Sehel amesema kuwa, mada mbalimbali zitawasilishwa katika mkutano huo ni pamoja na Majaji wanawake wanaongoza na kuleta mabadiliko katika Mahakama za Kimataifa, Wanawake katika Uongozi-Mahali pa Kazi Usalama kwa Maafisa wa Mahakama, Ubaguzi na biashara haramu ya binadamu na nyingine.
Kwa mujibu wa ratiba ya Mkutano huo, mmoja wa washiriki watakaotoa mada ya ‘Athari za teknolojia katika masuala ya ukatili wa kijinsia’ ni Mhe. Edith Mwalukasa ambaye ni Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo Mwambao Bagamoyo.
Washiriki wa TAWJA wanaotarajia kuhudhuria mkutano huo ni baadhi ya wanachama ni kutoka kutoka Zanzibar, Dar es Salaam, Dodoma, Mbeya, Arusha, Tabora na Mikoa mingine ya Tanzania Bara.

Mkutano wa aina hii huwakutanisha pamoja Majaji na Mahakimu Wanawake Duniani kote na hufanyika kila baada ya miaka miwili na huwapa fursa Majaji hao kujadili masuala mbalimbali yanayohusu haki za wanawake, ukatili wa kijinsia, watoto na jamii kwa ujumla.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved

International Women’s Day

International Women’s Day

Today, as we celebrate the International Day of Women Judges, I am pleased to share an article that showcases the remarkable journeys of some inspiring women judges from Canada, El Salvador, the Republic of Korea, and a Deputy Registrar from the United Republic of Tanzania. These women share their paths in the judiciary and provide you with useful insights and advice. Their stories are a testament to the power of diversity and the important role women play in the judiciary around the world. At World Intellectual Property Organization – WIPO, we are committed to fostering an inclusive intellectual property (IP) and innovation ecosystem that supports innovation and creativity for the benefit of everyone, everywhere. Our WIPO Judicial Institute collaborates closely with judiciaries worldwide, providing tailored support that respects local traditions and enhances IP adjudication skills. These trailblazing women are not only advancing IP law within their regions but also inspiring future generations to join in building inclusive and dynamic IP systems.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved

MAJAJI, MAHAKIMU WANAWAKE WATOA ELIMU SIKU YA KIMATAIFA YA MAJAJI, MAHAKIMU MBEYA

MAJAJI, MAHAKIMU WANAWAKE WATOA ELIMU SIKU YA KIMATAIFA YA MAJAJI, MAHAKIMU MBEYA

Katika kusheherekea Siku ya Kimataifa ya Majaji na Mahakimu wanawake walitumia siku hiyo ya jana tarehe 10 Machi, 2025 kutoa elimu katika shule mbalimbali za Msingi na Sekondari za jiji la Mbeya.

Aidha, Shule zilizotembelewa katika zoezi hilo la utoaji elimu ni pamoja na Sangu High School, Samora Michel High School zilizopo katika Wilaya ya Mbeya na kutoa elimu kwa wanafunzi takribani 100,000 kutoka kwa waheshimiwa Majaji na Mahakimu Wanawake.

Waheshimiwa hao walitoa mada zilizoandaliwa na Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) zenye lengo la kuelimisha umma juu ya haki za msingi katika zama za kidigitali, huku wakifafanua mchango wa Majaji na Mahakimu Wanawake katika kushughulikia makosa ya unyanyasaji wa kimtandao kwa jinsia zote.

Waheshimiwa waliyoshiriki kutoa elimu hiyo walikuwa Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Atuganile Ngwala, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya Mhe Zawadi Laizer, Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Mwanjelwa Mhe. Angela Kannyaninyi Byera, Mhe. Joyce Massawe, Hakimu mkazi mahakama ya Mwanzo Mwanjelwa, Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Iyunga Mhe. Hafsa Shelimo na Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Mbeya Mjini Mhe. Miriam Kamwaga.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved

Uzinduzi wa wiki ya sheria

TAWJA GALA DINNER 2025

TAWJA DODOMA, MOROGORO WAMPONGEZA JAJI LATIFA MANSOOR

TAWJA DODOMA, MOROGORO WAMPONGEZA JAJI LATIFA MANSOOR

Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) Dodoma na Morogoro wamepongeza Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Mhe. Latifa Alhinai Mansoor baada ya kuapishwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hafla ya uapisho iliyofanyika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 22 Januari, 2025.

Mhe Jaji Mansoor aliteuliwa tarehe 10 Januari, 2025 na Mhe. Rais Samia kuwa Jaji wa Mahakama hiyo. Kabla ya uteuzi huo, Jaji Mansoor alikuwa Jaji Mfawidhi, Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC), Morogoro.

Akizungumza na wanachama wa TAWJA kwa Mkoa wa Dodoma na Morogoro Mhe. Jaji Mansoor   amewashukuru wanachama hao kwa upendo na ushirikiano wao waliouonesha kwake.

“Namshukuru Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema kwa neema yake ya kunifanya nimetambuliwa na kunifanya niwe hivi nilivyo leo, sijui tamaduni za kule lakini ninaahidi nitafanya kazi kwa bidii kubwa ninamuomba Mwenyezi Mungu anipe afya ya kutosha ili niweze kutimiza majukumu yangu ipasavyo hasa kusimamia ukuaji, uboreshaji na utendaji kazi wa Mahakimu,” amesema Mhe. Jaji Mansoor.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo fupi Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo amempongeza Mhe. Mansoor na kumtakia kila lakheri katika majukumu yake, na kumuomba apokee zawadi ambayo ameandaliwa na wanachama wa TAWJA wa Mkoa wa Dodoma.

Akizungumza kwa niaba ya TAWJA Morogoro pamoja na watumishi wa Morogoro Naibu Msajili wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC), Morogoro Mhe. Susan Kihawa amempongeza Mhe. Jaji Mansoor kwa kuteuliwa kushika nafasi hiyo na kuahidi wataendeleza yale mazuri ambayo amewaachia.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na baadhi ya watumishi kutoka Dodoma na Morogoro.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved

MBIO MIAKA 25 YA TAWJA ZAFANA ARUSHA

MBIO MIAKA 25 YA TAWJA ZAFANA ARUSHA

Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) leo tarehe 19 Januari, 2025 kimefanya mbio maalum zilizohusisha Majaji, Naibu Wasajili, Mahakimu, vikundi vya riadha pamoja na Wadau mbalimbali ili kupinga vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 25 tangu kuanzishwa kwake.

Mbio hizo ambazo zilijumuisha umbali wa kilomita tano, 10 na 21 zilianza majira ya saa 12:30 Asubuhi kwenye viwanja vya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) na kuongozwa na Mgeni Rasmi, Mhe. Shally Joseph Raymond, Mbunge na Mwenyekiti wa Wabunge wanawake Bunge la Tanzania na pia Mwenyekiti wa Bunge la Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) ambaye amemwakilisha Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson pamoja na  Mlezi wa TAWJA, Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma.

Akitoa salaam mara baada ya kumalizika kwa mbio hizo, Mwakilishi huyo wa Mgeni Rasmi, Mhe. Shally Joseph Raymond amesema mila gandamizi kama ndoa za utotoni, ukeketaji wa wanawake (FGM), umiliki wa ardhi, nafasi za uongozi na maamuzi bado ni vikwazo katika kufikia usawa wa kijinsia na kwamba mila na tamaduni potofu ni changamoto kubwa inayosababisha kufisha ndoto za wengi katika kujiletea maendeleo ya kweli.

“Juhudi za pamoja na mbinu mbalimbali za kujikwamua kutoka katika madhila haya zinafanyika ili kubomoa mifumo gandamizi na kuvunja minyororo iliyojikita katika jamii zetu kwa karne nyingi. Hivyo, jubilei ya TAWJA ni tukio linalostahili kusherehekewa, siyo tu kwa sababu ya umri bali dira na dhima ya Chama tangu awali, ya kuwa mshumaa  wa mwanga na matumaini, ikipigania haki za kijinsia, hususani za wanawake na watoto,” amesema Mhe. Shally. 

Ametoa rai kwa TAWJA kuwa, inapoadhimisha miaka 25 pamoja na kujivunia mafanikio ni vema pia kutafakari kwa pamoja changamoto zinazoikabili jamii kwa kuwa bado kuna mila, tamaduni na mifumo gandamizi na nyingi zikiwa zimepitwa na wakati na vilevile wanawake na watoto bado wapo nyuma katika kulinda na kuteteta haki zao za msingi.

“Ni heshima kubwa sana kwangu kusimama mbele yenu leo, kama Mgeni Rasmi, katika tukio hili adhimu lililoandaliwa na Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA). Leo, hatushiriki tu katika mbio hizi bali ni sehemu ya harakati zinazolenga kuleta mabadiliko, kuzindua uelewa na kupinga masuala ya ukatili wa kijinsia (GBV) yaliyoshamiri na kukithiri katika jamii yetu,” ameeleza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA), Mhe. Barke Sehel amesema mbio hizo ni ishara ya kuanza kwa maadhimisho ya Jubilei ya miaka 25 ya TAWJA, pamoja na kuwashirikisha, kuhamasisha na kujenga uelewa kwa jamii na umma kuhusu hatua za kuchukua dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia (GBV) dhidi ya wanawake na Watoto.

“Ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa jamii ya Tanzania ina haki na inazingatia usawa kwa wote. Hivyo, tukio la leo, linathibitisha kwamba hatuko peke yetu katika kusimamia haki na usawa. Ni faraja kwangu kuona kuwa kwa pamoja tumeweza na tunaweza kuleta mabadiliko na kuhakikisha kuwa kila mwanamke na mtoto nchini Tanzania anapata haki na fursa anayostahili,” amesema Mhe. Sehel.

Mwenyekiti huyo amebainisha kuwa, TAWJA imekuwa ikijikita kwenye kukuza haki za binadamu na usawa kwa wote, hususan kwa wanawake, watoto na makundi maalum na kwamba wanapoadhimisha Jubilei ya miaka 25, TAWJA inajivunia kwa hatua kubwa ilifokia kwani imeweza kuletea mchango chanya kwenye jamii kwa upande wa haki.

Mhe. Sehel ameongeza kuwa, Chama hicho kimechangia kwenye mabadiliko ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, na kueleza kuwa, “TAWJA ilichukua juhudi za makususdi za kutoa elimu kwa wadau wa haki jinai, wabunge na jamii, kuhusu rushwa ya ngono (sextortion) na hivyo kuleta uelewa mpana katika jamii juu ya uwepo na athari ya vitendo vya rushwa ya ngono na hatimaye kubadilishwa kwa sheria kwa kuongeza kifungu maalum kuhusiana na rushwa ya ngono.”

Amesema baada yam bio hizo, wamepanga kutembela Shule za Sekondari sita, ambazo ni Ilboru, Arusha, Kimandolu, Kaloleni, Muriet na Sinoni kwa ajili ya kuanzisha Klabu za Haki za Kijinsia Mashuleni (Gender Justice Clubs) ambapo Wanachama wa TAWJA watapata fursa ya kutoa elimu kwa wanafunzi kuhusu kutambua aina zote za ukatili wa kijinsia, jinsi na wapi ya kuripoti ukatili wa kijinsia na kuwapa ujuzi muhimu wa maisha ikiwemo kuweka malengo ya kibinafsi na kujali afya na usafi wao.  

Mwenyekiti huyo ametoa shukran kwa Mahakama ya Tanzania, Mahkama ya Zanzibar, Kamati ya Maandalizi, wanachama wa TAWJA, wadau ambao ni UN Women, UNDP, WCF, PSSSF, Benki ya Equity, Jeshi la Polisi na Magereza, Hospitali ya Moyo, Vyama vya Riadha na wananchi wote waliojumuika kuungana nao na kufanikisha tukio hilo muhimu.

Mbio hizo zimebeba kaulimbiu, “Mshikamano katika Haki za Kijinsia Huanzia Hapa: “Shiriki na Elimisha.” Sambamba na hilo katika maadhimisho ya miaka 25 ya TAWJA kuna mabanda ya wadau mbalimbali likiwemo la Chama hicho ambao wanatoa elimu kuhusiana na huduma zao.

Ufunguzi wa Maadhimisho ya miaka 25 ya TAWJA unatarajiwa kufanyika kesho tarehe 20 Januari, 2025 ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved

MAJAJI, MAHAKIMU WANAWAKE TANZANIA KUSHIRIKI MKUTANO WA ‘IAWJ’ ACCRA GHANA

MAJAJI, MAHAKIMU WANAWAKE TANZANIA KUSHIRIKI MKUTANO WA ‘IAWJ’ ACCRA GHANA

Majaji na Mahakimu Wanawake wa Mahakama ya Tanzania wanatarajia kuungana na Majaji wanawake wenzao kutoka Ukanda wa Afrika kushiriki katika Mkutano wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Duniani (IAWJ) utakaofanyika jijini Accra nchini Ghana.

Akizungumza katika mahojiano maalum leo tarehe 12 Mei, 2024, Mwenyekiti wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) ambaye pia ni Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Barke Sehel amesema kuwa, Mkutano huo unatarajiwa kuanza rasmi kesho tarehe 13 hadi 18, Mei, 2024 na utafunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Ghana, Mhe. Nana Addo Dankwa Akufo-Addo.

“Mkutano huu ni wa Kikanda kwa Chama cha Majaji na Mahakimu wanawake, Mkutano huu unakutanisha wanachama Majaji na Mahakimu wanawake Afrika kwa ujumla. Kwa upande wa Tanzania tutakaoshiriki katika Mkutano huo ni 18 na idadi hii imejumuisha na wenzetu wa Zanzibar,” amesema Mhe. Sehel.

Mwenyekiti huyo ameeleza kwamba, katika Mkutano huo, Mahakama ya Tanzania itapata nafasi ya kutoa mada ya kuelezea hatua zinazochukuliwa na TAWJA katika kumpa nafasi mwanamke kwenye Uongozi hasa kwenye Mahakama.

Kaulimbiu ya Mkutano huo inasema ‘Nafasi ya Majaji Wanawake katika kupambana na mila potofu katika ulimwengu wa sasa.’

Mbali na TAWJA, Vyama vingine vitakavyoshiriki katika mkutano huo ni kutoka Nigeria, Kenya, Uganda, Afrika Kusini, Cote d’Ivoire na nyingine.

Kiongozi wa msafara wa wanachama wa TAWJA, Mhe. Sehel pamoja na wenzake wamewasili leo hii jijini Accra majira ya saa 5 asubuhi tayari kwa kushiriki kikamilifu Mkutano huo muhimu.

© 2024 Tanzania Women Judges Association. All Rights Reserved